Top News

Obama Aibuka na Onyo Kali Baada ya Trump Kusaini Makubaliano Mapya na Iran

Rais wa Marekani Donald Trump ameyasifu makubaliano mapya kati ya Marekani na Iran, akiyataja kama ushindi mkubwa wa diplomasia na usalama wa kimataifa, huku akiyalinganisha na makubaliano ya nyuklia ya mwaka 2015 yaliyoongozwa na Rais wa zamani Barack Obama.

Akizungumza katika taarifa zake, Trump alidai kuwa makubaliano hayo mapya ni hatua kali zaidi dhidi ya Iran, yakilenga kuhakikisha Tehran haitawahi tena kuendeleza uwezo wa kutengeneza silaha za nyuklia. Alikosoa vikali makubaliano ya JCPOA ya 2015, akisema yalikuwa na mapungufu makubwa na yaliipa Iran nafasi ya kuendeleza mipango yake ya nyuklia kwa njia fiche.

Makamu wa Rais JD Vance ameongeza uzito wa kauli hiyo, akisema mpango wa nyuklia wa Iran umeangamizwa kikamilifu na kwamba makubaliano mapya yatakuwa kinga ya kudumu dhidi ya jaribio lolote la Tehran kurejea kwenye uundaji wa silaha za nyuklia. Kwa mujibu wa Vance, rasimu ya makubaliano hayo yenye vipengee 14 ilitarajiwa kuwekwa wazi kabla ya kutiwa saini rasmi Ijumaa.

Hata hivyo, mjadala mkubwa umeibuka kuhusu tofauti kati ya makubaliano haya mapya na yale ya mwaka 2015 (JCPOA), yaliyosimamiwa na utawala wa Barack Obama kwa kushirikiana na mataifa makubwa duniani.

Katika makubaliano ya 2015, Iran ilikubali kupunguza kiwango cha urutubishaji wa urani hadi asilimia 3.67, kiwango kinachoruhusu matumizi ya kiraia pekee, sambamba na kuondolewa kwa baadhi ya vikwazo vya kiuchumi dhidi yake. Makubaliano hayo yalikuwa ya kina, yakihusisha nchi sita kubwa duniani pamoja na Iran. SOMA ZAIDI.

Post a Comment

Previous Post Next Post