Siku mia moja tangu kuanza kwa mivutano ya kivita dhidi ya Iran, Rais Donald Trump anaonekana kukwama katika juhudi zake za kushawishi umma wa Marekani kuunga mkono harakati hizo.
Kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa na kituo cha habari cha Al Jazeera, utafiti mpya uliofanywa na Chuo Kikuu cha Maryland kuhusu masuala tete ya kitaifa, umebaini hali ya kutoamini na kutilia shaka mwelekeo wa Marekani katika mgogoro huo.
Matokeo ya utafiti huo yaliyowekwa wazi Alhamisi iliyopita, yanaonyesha kuwa ni asilimia 16 tu ya wapiga kura nchini Marekani wanaoamini kuwa nchi hiyo imepata ushindi au iko kwenye mkondo wa kushinda vita hivyo dhidi ya Iran.
Kukosekana kwa uungaji mkono wa umma na kutoaminika kwa mikakati ya kijeshi inayotumiwa na serikali, kumetajwa kama tishio kubwa kwa mustakabali wa kisiasa wa Rais Trump.
Kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa na kituo cha habari cha Al Jazeera, utafiti mpya uliofanywa na Chuo Kikuu cha Maryland kuhusu masuala tete ya kitaifa, umebaini hali ya kutoamini na kutilia shaka mwelekeo wa Marekani katika mgogoro huo.
Matokeo ya utafiti huo yaliyowekwa wazi Alhamisi iliyopita, yanaonyesha kuwa ni asilimia 16 tu ya wapiga kura nchini Marekani wanaoamini kuwa nchi hiyo imepata ushindi au iko kwenye mkondo wa kushinda vita hivyo dhidi ya Iran.
Kukosekana kwa uungaji mkono wa umma na kutoaminika kwa mikakati ya kijeshi inayotumiwa na serikali, kumetajwa kama tishio kubwa kwa mustakabali wa kisiasa wa Rais Trump.
Wachambuzi wa masuala ya kisiasa nchini humo wametahadharisha kuwa, hali hii ya kutoridhika kwa wananchi inaweza kukidhoofisha Chama cha Republican na kukisababishia pigo kubwa katika uchaguzi ujao.
Kushuka huku kwa umaarufu wa kampeni hiyo ya kijeshi kunaashiria mpasuko mkubwa kati ya sera za nje za utawala wa Trump na matarajio ya wapiga kura, ambao sasa wanaonekana kuwa na wasiwasi na gharama pamoja na matokeo ya muda mrefu ya vita hivyo. SOMA ZAIDI.
Kushuka huku kwa umaarufu wa kampeni hiyo ya kijeshi kunaashiria mpasuko mkubwa kati ya sera za nje za utawala wa Trump na matarajio ya wapiga kura, ambao sasa wanaonekana kuwa na wasiwasi na gharama pamoja na matokeo ya muda mrefu ya vita hivyo. SOMA ZAIDI.
Post a Comment